Linda afya ya Moyo kwa kufanya hivi
Miongoni mwa magonjwa ambayo husumbua watu wengi kwa kiwango kikubwa ni
moyo, hivyo ili kuweza kulinda afya ya moyo wako ili usipate magonjwa
hayo ya moyo unatakiwa kufanya yafuatayo;
- Pima shinikizo la damu angalau mara moja kwa mwaka.
- Hakikisha unakuwa na uzito sahihi.
- Fanya mazoezi walau nusu saa kwa siku.
- Punguza matumizi ya chumvi kwenye chakula. Hapa tunanzungumzia chumvi ya mezani ambayo huongezwa kwenye vyakula kama vile nyama choma, chipsi n.k
- Kila wakati hakikisha unakula zaidi matunda,mboga za majani na vyakula ambavyo havina mafuta.
- Punguza matumizi na unjwaji wa pombe.
- Iwapo umegundulika kuwa na tatizo la shinikizo la damu,tumia dawa kama ulivyoelekezwa na watalamubwa afya na si vinginevyo.

Maoni
Chapisha Maoni