MGOGORO BAINA YA MWEKEZAJI WA KIWANDA CHA SUKARI CHA TPC DHIDI YA WANANCHI WAPATIWA UFUMBUZI


MOSHI.

WAZIRI wa maji  na Umwagiliaji Mhandisi, Isack Kamwelwe amepata mwarubaini  wa changamoto  ya mgogoro  wa maji baina ya  Mwekezaji wa kiwanda cha sukari cha TPC na wakulima wa maeneo hayo baada ya kukaa na kufanya mazungunzo  na pande zote mbili.
Waziri huyo alisema baada ya mazungunzo na pande hizo mbili alibaini chanzo cha mgogoro huo ni maji ambayo  hayatoshi  kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi  na kusema serikali imeona ipo haja ya kuchimba visima vikubwa na kujenga mabwawa makubwa  ya kuifadhi maji nyakati za mvua ili kunusuru mgogoro huo.
Ziara hiyo  iliyifanyika jana ambapo Waziri huyo alifika katika kiwanda cha Tpc  ikiwa na lengo la kutimiza agizo la Rais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli  lililomtaka waziri huyo kuhakikisha ametatua mgogoro huo ndani ya siku 7, alilolitoa katika kikao cha wafanyabiasha kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es salam mwishoni mwa wiki iliyopita.
“Nimekaa na  pande zote mbili nimewasikiliza na kubaini ya kuwa maji ya umwagiliaji yanayotumika na wakulima  wa Ongama  na Mwekezaji wa TPC  hayatoshi kutokana na wakulima  kulima kwa kiwango kikubwa na mabadiliko ya tabia nchi… hivyo  serikali imeona usuluwishi wa kudumu ni kuhakikisha tunashirikiana na mwekezaji kwa kuchimba  visima vikubwa,”alisema  na kuendelea kuwa.
“Sanyari na kuchimba visima hivyo virefu  pia kujenga bwawa kubwa katika maeneo ya Miwaleni  kata ya Kahe Wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro kutokana na kubaini eneo lile ni tambarare  na maji mengi hupote bure wakati wa mafuriko hivyo yanaweza yakawasaidia wakulima wakati wa kiangazi,” alisema Waziri.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MHANDISI ISACK KAMWELWE.
 
Aidha Waziri huyo  alitoa  siku sita  kwa Ofisi  ya Bonde la Mto Pangani kuwasilisha idadi ya wakulima walioko katika mradi wa umwagiliaji na  kiasi cha maji  kinachohitajika ili kuona namna ya kutatua tatizo hilo kwa urahis zaidi.

“Sisi kama serikali tunapongeza  wakulima waliowekeza kwa kulima mashamba makubwa kutoka Hekta 300 hadi  wanakaribia Hekta 2000  ikiwa wanatekeleza Serikali ya viwanda lakini pia tunampongeza mwekezaji  kwa kusaidia kwa asilimia kubwa mapato ya nchi hivyo wote ni muhimu kwetu  …. bonde hakikisheni mnaleta taarifa hiyo mapema iwezekanavyo ili kutatua changamoto hiyo,”alisema Waziri.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Utawala wa kiwanda cha Sukari cha TPC, Jaffary  Ally alikiri kuwepo kwa mgogoro huo kwa zaidi ya miaka 10 sasa na kusema wapo tayari kushirikiana na serikali kuchimba visima hivyo ambavyo vitasaidia kumalizaka kwa mgogoro huo.

AFISA MTENDAJI WA UTAWALA WA KIWANDA CHA SUKARI CHA TPC, JAFFARY ALLY.
 
Alisema kwa Mujibu wa kipima maji  kiwanda cha TPC kinahitajika kutumia  lita 1700 kwa sekunde  huku wakulima wakihitajika kutumia  lita 900 kwa sekunde ambapo hadi kufikia sasa TPC hutumia maji lita 1000 tu kwa sekunde kutokana na wakulima kuongezeka mashamba kutoka hekta  300 hati hekta takribani 900.

Naye mkuu wa wilaya ya Moshi , Kippi Warioba   alisema changamoto za mgogoro huo zipo na  yeye kama msimamizi wa ulinzi na usalama  kwenye wilaya hiyo atahakikisha uharibifu wa miundombinu haufanyiki.
Aidha Afisa mtendaji wa Kata ya Tpc Arusha Chini, Jane Mandara, alikiri kuwepo kwa changamoto ya  maji hali inayopelekea migogoro baina ya mwekezaji na wakulima.

“Tunaiomba serikali kuangalia uwezekano wa kuchimba maji ya chini  ili kuweza kusaidia kupata kila mmoja haki za maji na kuweza kuendelea na shughuli za uzalishaji,”alisema Mtendaji Jane.

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ufahamu ugonjwa wa Ngiri ( Hernia) kiundani zaidi

Mama ajifungua mapacha wenye baba tofauti

UVCCM SIHA YAZINDUA KAMPENI YA KUGAWA TAULO ZA KIKE KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI