MUWSA YAJIDHATITI KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA
MOSHI.
MAMLAKA ya maji safi na usafi wa
mazingira Moshi(MUWSA) imetenga vyanzo vitatu vya maji ambavyo vinauwezo wa
kuzalisha mita za ujazo 12000 kwa siku ambapo maji hayo yanategemewa
kuhudumia shughuli za matumizi ya viwanda.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa
mamlaka hiyo Joyce Msiru alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na waandishi
wa habari ofisini kwake kuhusiana na jinsi mamlaka hiyo ilivyojipanga
kuhakikisha viwanda vinapata huduma ya maji muda wote.
MKURUGENZI WA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA), JOYCE MSIRU.
Alisema kuwa, mamlaka hiyo tayari
imeshavitenga vyanzo hivyo vitatu na kwa sasa wameshapata vibali vya kuvitumia.
Msiru alidai kuwa vyanzo hivyo
vitatu vinapatikana ndani ya mto Kikavu ambapo vitasaidia kuongeza upatikanaji
wa maji katika maeneo ya viwanda.
"Mamlaka imeweka mikakati
mbalimbali wakati tunaelekea kwenye nchi ya viwanda hivyo kutakuwa na
tawi maalumu ambalo litakuwa mahususi kwa ajili ya viwanda pekee yake,"
alisema.
Alisema kuwa mamlaka imefikia
malengo ya 2020/25 ambayo yalitaka upatikana wa maji kwa mji wa Moshi uwe ni
kwa asilimia 100 ambayo imeshafikiwa na mamlaka hiyo kwa sasa.
Akizungumzia suala wadaiwa sugu
wa ankra za maji Msiru alisema kuwa tayari wameshafanya mazugumzo na taasisi
hizo ambazo zinadaiwa.
"Ni kweli taasisi za
serikali ikiwemo, Gereza kuu la Karanga, ofisi ya RPC na shule ya polisi Moshi,
tunawadai lakini tumeshaanza kufikia hatua nzuri ya kufikia muafaka,"
alisema.
AFISA UHUSIANO WA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA),RASHIDI NACHAN.
Mkurugenzi wa manispaa ya Moshi
Michael Mwandenzi,alisema upatikanaji wa maji safi na usafi Manispaa ni kwa
asilimia 99.
"Wanachi wa manispaa
ya Moshi wanapata maji safi na salama kwa asilimia zaidi ya aslimia 99 hakuna
mwananchi wa moshi anayefuata maji kwa zaidi ya kilometa moja," alisema
Mwandenzi alisema kuwa miongoni
mwa vigezo vinavyoangaliwa kwenye tuzo za usafi ni pamoja upatikanaji wa maji
safi na salama na kwamba maji Moshi yapo kwenye viwango vya ubora wa kimataifa.
Mwisho....


Maoni
Chapisha Maoni