MUWSA YAKABIDHIWA MITI 7000…..




MOSHI.

MRADI wa Trees’ 4 Kili umetoa msaada wa miti 7000 kwa Mamalaka ya maji safi na maji taka mjini Moshi kwa ajili ya kupanda katika vyanzo vya maji ili kukabiliana na upungufu wa maji na athari za mazingira na kijamii mjini Moshi.

Mkurugenzi wa mradi wa Tree’4 Kili Thomas Munuo amesema hayo jana katika zoezi la upandaji wa miti katika chanzo cha maji cha Kaloleni kilichopo mjini Moshi na kuongeza kuwa mradi huo unakusudia kupanda miti zaidi ya milioni Moja mwaka huu.

Amesema wanakusudia kutoa bure miche ya miti ya miti kwa taasisi binafsi, serikali zikiwemo Hospitali,vyuo ,shule za sekondari na msingi,makanisa na misikiti na kwamba zoezi hilo litakuwa endelevu.

Munuo alisema mradi wa Trees 4 Kili umeamua kutoa msadaa wa miche ya miti kwa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini hapa (MUWSA) na klabu ya Moshi  ili kutunzamazingira na vyanzo vya maji.

Amesema mradi wa Trees 4 Kili unakusudia kupanda miti zaidi ya Milioni hamsini mkoani Kilimanjaro ili kukabiliana na athari za mazingira na kijamii mkoani Kilimanjaro kwani kupungua kwa theluji na mvua,kuongezeka kwa joto vinachangiwa na zoezi la ukataji miti ovyo.

Munuo alisema mradi wa Trees’4 kili umeanzishwa mkoani Kilimanjaro  kwa lengo la kukabiliana na athari za mazingira na kijamii na kushukuru  kampuni ya bia nchini (TBL) kusaidia mpango wa kukusanya fedha  kwa ajili ya zoezi la upandaji  miche ya miti 100,000.

Mkurugenzi wa Maji safi na maji taka (MUWSA) Joyce Msiru alisema Mamlaka yake inakusudia kupanda miche ya miti zaidi ya 12,000 kwa mwaka huu katika vyanzo vya maji vilivyopo mjini Moshi.

Mkuu wa wilaya ya Moshi Kippi Warioba akiendesha zoezi la upandaji wa miti katika chanzo cha maji cha kaloleni alitoa wito kwa wananchi kuuunga mkono jitihada za serikali katika kukabiliana na tatizo la uharibifu wa mazingira kwa kuacha kufanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji.

Mkuu huyo wa wilaya alisema ni marufuku kwa mtu yoyote kujenga nyumba za makazi na kulima karibu na vyanzo vya maji kwani sheria zinazuia kufanya shughuli za kipinadamu ndani ya mita sitini kutoka katika vyanzo vya maji na kwamba serikali haita sita kumchukulia sheria mwananchi yoyote atakayekiuka sheria hiyo.

Mwisho…

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ufahamu ugonjwa wa Ngiri ( Hernia) kiundani zaidi

Mama ajifungua mapacha wenye baba tofauti

UVCCM SIHA YAZINDUA KAMPENI YA KUGAWA TAULO ZA KIKE KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI