SERIKALI IMEJIPANGA KUMALIZA KERO ZA WALIMU…
KATIBU TAWALA WA MKOA WA KILIMANJARO, MHANDISI AISHA AMOUR (wa pili kulia),AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAJUMBE NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WALIMU MKOA WA KILIMANJARO (wa kwanza kushoto) MWENYEKITI WA CWT MKOA, OMARY MCHOMVU AKIFUATIWA NA KATIBU WA CWT MKOA, DIGNA NYAKI NA WA KWANZA KULIA NI MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI TAIFA, SALMA KIMARO.
MOSHI.
KATIBU Tawala mkoa wa Kilimanjaro,
Mhandisi Aisha Amour amesema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa
changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu zinapatiwa ufumbuzi huku
akishitushwa na tatizo la walimu mkoa hapa kucheleweshewa mafao yao ya
kustaafu.
Mhandisi Amour alitoa kauli hiyo katika
baraza la dharura la chama cha Walimu (CWT), mkoa wa Kilimanjaro ambapo alisema
kuwa, Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa walimu katika kuchangia maendeleo ya
Taifa.
“Serikali inatambua changamoto
mbalimbali ambazo nyinyi walimu mmekuwa mkikabiliana nazo ikiwamo madeni yenu
lakini zipo juhudi mbalimbali ambazo zimefanywa na serikali ili kuhakikisha
kuwa changamoto zote zinapatiwa ufumbuzi hivyo msife moyo tambueni serikali ipo
pamoja na nyie” alisema Mhandisi Amour.
Katibu Tawala huyo wa mkoa
alisikitishwa na changamoto ya walimu katika mkoa wa Kilimanjaro kucheleweshewa
mafao yao ya wastaafu na kudai kuwa Serikali ilishakataza ucheleweshaji wa
mafao kwa watumishi wanaostaafu hali iliyompelekea kukitaka chama cha walimu
mkoa kumwandikia orodha ya majina ya walimu waliocheleweshewa mafao ili aweze
kulishughulikia.
Akizungumzia swala la Walimu wa
Sekondari kuhamishwa kwenda kufundisha shule za msingi alisema kuwa, yapo
malalamiko mbalimbali yaliyotolewa na walimu katika zoezi hilo ambapo wapo
baadhi ya Watumishi wa halmashauri mkoa Kilimanjaro wamekuwa wakitumia kigezo
cha kuwakomoa walimu kutokana na chuki binafsi.
Alisema kuwa kwa sasa ameunda tume
maalum ambayo imeanza kupita kila halmashauri ili kujua jinsi zoezi la
kuwahamisha walimu kutoka sekondari kwenda kufundisha shule za msingi jinsi
lilivyofuata kanuni na vigezo vilivyowekwa.
Aidha Mhandisi Amour alisema kuwa,
Walimu wengi wamekuwa wakiilaumu Serikali kutokana na baadhi ya Watendaji wa
halmashauri kutotimiza wajibu wao na kudai kuwa hata mvumilia Mtendaji yeyote
wa Serikali katika mkoa huo atakayekiuka matakwa ya Serikali na kupelekea
kuingia katika lawama.
Akizungumzia tatizo la baadhi ya halmashauri
kuwaondoa walimu katika malipo alisema kuwa limekuwa tatizo kubwa hali ambayo
imemlazi kuunda timu maalum ambayo imekuwa ikipita kila halmashauri kuchukua
majina ya walimu walioondolewa pamoja na sababu za kuwaondoa ili kujua nini
tatizo na kuomba kupewa muda ili aweze kulitolea ufafanuzi baada ya kupata
majinu ya tume hiyo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama
cha walimu mkoa wa Kilimanjaro, Omary Mchomvu alisema kuwa, hakuna watu wenye
nidhamu kama walimu kama wakitendewa haki zao za msingi na kutumia nafasi hiyo
kuiomba serikali kutimiza matakwa ya walimu.
Mchomvu alisema kuwa, walimu katika
mkoa wa Kilimanjaro amekuwa wakiwajibika kwa vitendo na hiyo imejidhihirisha
baada ya mkoa kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya kidato cha nne
na kudia kuwa chama chao kimejipanga kuhakikisha mkoa unaendelea kushika nafasi
hiyo.
Awali akisoma risala ya Walimu kwa
Katibu Tawala, Katibu wa CWT mkoa wa Kilimanjaro, Digna Nyaki alisema kuwa,
walimu wa mkoa wa Kilimanjaro wanakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Nyaki alisema kuwa miongoni mwa
changamoto hizo ni pamoja na walimu waliohamishwa kutoka shule za sekondari
kwenda shule za msingi mkoani hapa wamehamishwa bila kulipwa gharama zao za
uhamisho kinyume na kauli ya Rais Dk. John Pombe Magufuli aliyotoa Desemba
mwaka jana mjini Dodoma.
Dk. Magufuli akifungua mkutano mkuu
wa chama cha walimu Taifa Dodoma
KATIBU WA CWT MKOA WA KILIMANJARO, DIGNA NYAKI.
alisema kuwa, mwalimu asihamishwe bila mwajiri
kuwa na fedha ya kumlipa lakini katika hali ya kushangaza waajiri wamekuwa
wakifanya hivyo.
Alisema kuwa, changamoto nyingine ni
kutolipwa kwa deni lao shilingi Bilioni 1.131 ambapo deni hilo ni kwa walimu wa
mkoa wa Kilimanjaro pekee ambayo sio ya mishahara na yalishahakikiwa na
serikali kwa kushirikiana na chama cha walimu.
Mwisho….
WAJUMBE WA BARAZA LA CHAMA CHA WALIMU MKOA WA KILIMANJARO WAKIFUATILIA KWA MAKINI HOTUBA YA MGENI RASMI KATIKA BARAZA HILO AMBAYE NI KATIBU TAWALA WA MKOA WA KILIMANJARO, MHANDISI AISHA AMOUR (HAYUPO PICHANI)MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI TAIFA, SALMA KIMARO AKIMPA ZAWADI ILIYOANDALIWA NA WALIMU MGENI RASMI KATIKA BARAZA HILO AMBAYE NI KATIBU TAWALA WA MKOA WA KILIMANJARO, MHANDISI AISHA AMOUR.
KATIBU WA CHAMA CHA WALIMU MKOA WA KILIMANJARO, DIGNA NYAKI AKIFURAHIA JAMBO MARA BAADA YA KUHITIMISHA BARAZA HILO JANA.








Maoni
Chapisha Maoni