TRA YAINGIZA MILIONI 368.77 KUTOKANA NA BIDHAA ZA MAGENDO ..




MOSHI.

MAMLAKA ya Mapato nchini TRA, mkoa wa Kilimanjaro imekusanya kiasi cha shilingi milioni 368.77 kama kodi na faini za bidhaa mbalimbali zilizoingizwa nchini kinyume na sheria katika kipindi cha Julai mwaka jana hadi Februari mwaka huu.

Hayo yalibainishwa na Meneja msaidi wa mamalaka hiyo mkoa wa Kilimanjaro anayeshughulikia maswala ya forodha, Godfrey Kitundu wakati alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kudai kuwa, wapo baadhi ya Wananchi ambao sio waaminifu wamekuwa wakiingiza nchini bidhaa za magendo.

Kitundu alisema kuwa, Wafanyabiashara hao wamekuwa wakitumia njia zisizo rasmi (njia za panya), kupitisha bidhaa hizo ambapo katika mkoa wa Kilimanjaro zipo njia zisizo rasmi zipatazo zaidi ya 300.

Alisema kuwa, mkoa wa Kilimanjaro unapakana na nchi jirani ya Kenya ambapo unanjia halali tatu zilizohidhinishwa na Serikali ambazo ni Holili, Tarakea na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambazo ndizo njia zilizopendekezwa na Serikali kupitisha mizigo mbalimbali.

Meneja huyo alibainisha kuwa, bidhaa ambazo zimekuwa zikiingizwa nchini kwa njia za magendo ni Sukari inayozalishwa kutoka nchini Brazili na Msumbiji ambapo tokea mwezi Desemba mwaka jana paka sasa jumla ya Tani 41 sawa na kilogramu 4100, imeshakamatwa ambapo paka sasa wanaishikilia.

Aliendelea kudai kuwa, bidhaa nyingine ni mafuta ya taa ambapo kuanzia mwezi Julai mwaka jana paka sasa jumla ya lita 27000 zilikamatwa, chumvi zikiwa katoni 2000 na bidhaa ndogo ndogo kama pipi zikiwa katoni 397.

“Wapo baadhi ya wafanyabiashara ambao sio waaminifu wamekuwa wakiingiza bidhaa mbalimbali nchini kwa kutumia njia zisizo rasmi huku wakitambua kuwa kufanya hivyo ni kuhujumu uchumi wa nchi na kuvizorotesha viwanda vya ndani” alisema Kitundu.

Meneja huyo aliendelea kudai kuwa, bidhaa hizo zimekuwa zikiingizwa nchini kwa kutumia usafiri wa pikipiki na magari ambapo toka mwezi  Julai mwaka jana paka sasa jumla ya pikipiki 52  na magari 17 yalikamatwa yakiingiza bidhaa za magendo nchini.

Kwa mujibu wa sheria za nchi chombo chochote cha usafiri kikikamatwa kikiwa kinasafirisha bidhaa za magendo adhabu yake ni kukitaifisha.

Aidha Meneja huyo alisema kuwa, TRA wamekuwa wakishirikiana na vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama wakiwamo jeshi la Polisi na Wananchi wenye nia njema na Taifa katika kuwabaini na kuwakamata wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiingiza bidhaa hizo za magendo nchini.

Katika hatua nyingine alisema kuwa, kwa sasa wanakabiliwa na changamoto ya magari ya kufanyia operesheni katika eneo lote la mpaka, huku pia wamekuwa wakiendelea kuwaelimisha Wananchi kuacha tabia ya kupita njia za panya na badala yake wapiti njia rasmi na kulipa kodi kulingana na bidhaa alizonazo.

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ufahamu ugonjwa wa Ngiri ( Hernia) kiundani zaidi

Mama ajifungua mapacha wenye baba tofauti

UVCCM SIHA YAZINDUA KAMPENI YA KUGAWA TAULO ZA KIKE KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI