VIJANA WATAKIWA KUWEKEZA KWENYE VIWANDA


MOSHI.


UMOJA wa vijana ya chama Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa kilimanjaro umewataka vijana kuwekeza kwenye uchumi wa viwanda kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro Abdulrahimu Hamad,wakati akizungumza na umoja wa vijana wilaya wa Moshi vijijini ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya viongozi was vijana mkoa kutembelea wilaya zote za mkoa huo na kukutana na Wajumbe wa mabaraza ya wilaya.

Alisema kuwa vijana wanapaswa kuchangamikia fursa za kuwekeza katika uchumi wa viwanda kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo.

"Tunakiwa kuwa kioo katika jamii kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo pia  kusimamia shughuli mbalimbali za kiuchumi,sisi wenyewe tunatakiwa tupate maendeleo kwanza,ili jamii inayotuzunguka waone faida ya kuwa ndani ya ccm," alisema.


"Vijana wanakiwa kuwa chemchemi za fikra ndani ya ccm,kwa kushiriki kikamilifu katika kutatua changamoto mbalimbali za kiuchumi na kijamii," alisema.


Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro,Ivan Mushi ,alisema ukosefu wa ajira kwa vijana iwe fursa ya kubuni ajira mpya kwa  vijana .

"Tuitumie changamoto ya huhaba wa ajira kama fursa za kubuni ajira na kujikwamua kiuchumi," alisema.

Alisema kuwa zipo njia nyingi za kujiajiri ikiwemo uwekezaji katika kilimo ,kutafuta tenda za ujenzi wa miradi mbalimbali.

"Nitatenga muda wakufanya ziara katika wilaya moshi vijijini ,na nitahakikisha kushirikiana kutatua kero za vijana," alisema.

Mwenyekiti UVCCM wilaya Moshi Hassan Husein alisema kuwa jumuiya hiyo ngazi ya wilaya haina fedha   za kuendesha shughuli hali inayowapelekea kushindwa kutekeleza majukumu mengine za kiutendaji.

Katika ziara hiyo yenye ujumbe wa "Yajayo yanafurahisha upo tayari?" Wameongozana na Mjumbe wa Baraza kuu la vijana Taifa, kupitia mkoa wa Kilimanjaro Nice Munissi, Mjumbe wa Mkutano mkuu Taifa, Said Mndeme, Katibu hamasa na chipukizi mkoa wa Kilimanjaro, Dickson Tarimo.


Mwisho...

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ufahamu ugonjwa wa Ngiri ( Hernia) kiundani zaidi

Mama ajifungua mapacha wenye baba tofauti

UVCCM SIHA YAZINDUA KAMPENI YA KUGAWA TAULO ZA KIKE KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI