WANANCHI WA WILAYA YA SAME WAKUMBUSHWA KUSHIKA LESEN ZA MADINI ILI KUNUFAIKA NA GYPSUM..


Mkuu wa wilaya ya Same mkoa Kilimanjaro, Rosemary Senyamule (wa tatu kushoto) akishirikiana na Wananchi wa kata ya Bendera wilayani Same kufeka barabara jana wakati alipofanya ziara katika kata hiyo kusikiliza kero za wananchi.

                                                            SAME



MKUU wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Rosemary Senyamule amewakumbusha wananchi wa wilaya hiyo kushika leseni za madini na kuanza kuchimba Gypsum kutoka na kubainika kuwa Gypsum inayopatika Same inaubora mkubwa kuliko maeneo mengine.

Senyamule alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Bendera ikiwa ni mwendelezo wa kusikiliza kero za wananchi katika wilaya hiyo ambapo alisema kuwa imebainika Gypsum inayopatikana wilaya ya Same inaubora mkubwa.

Alisema kuwa, Wananchi wa wilaya hiyo wanapaswa kuanza kuomba leseni za madini zitakazowaruhusu kuchimba Gypsum na kuondokana na tatizo la ajili ambalo limekuwa tatizo kwa vijana wengi.

“Tunatambua kuwa vijana wamekuwa wakilalamika kwa kukosa ajira sasa vijana wa same neema imekuja hivyo tunapaswa kuichangamkia kwa kuomba leseni ya madini na kuanza kunufaika na uchimbaji wa Gypsum” alisema Senyamule.

Aidha mkuu huyo wa wilaya aliuagiza uongozi wa kata hiyo kushirikiana kwa pamoja kutenga eneo lenye madini hayo kwa ajili ya vijana hali itakayopunguza tatizo la ajira.

Senyamule alisema kuwa, atakaa na idara ya madini ili waweze kwenda kuwapa elimu wananchi juu ya taratibu za kupata leseni za uchimbaji lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa hawacheleweshwi katika kupata leseni hiyo. 

Mkuu huyo wa wilaya alisikitishwa na tatizo la mgao wa maji ya Umwagiliaji ambalo lililalamikiwa na wananchi wa kata hiyo, na kutoa maagizo kwa wataalamu kumpa majibu ndani ya wiki mbili kuhusiana na mgao huo huku akiwataka kuhakikisha wanamaliza tatizo hilo ili wananchi waendelee na shughuli za kujipatia kipato.

Katika hatua nyingine alisikitishwa kusikia lipo tatizo la Wanafunzi kubakwa ambalo lilimkera na mara baada ya kutajiwa mtu anayehusika kuwafanyia wanafunzi kitendo hicho aliamuru jeshi la Polisi kumkamata na kumfungulia kesi haraka huku pia akiondoka na wanafunzi wa kike wapatao wanne waliofanyiwa kitendo hicho cha ukatili.

Pia aliwaasa viongozi wa kata kutowachelewesha wananchi kwenye maendeleo na badala yake washirikiane kwa pamoja bila kujali itikadi ya vyama kwani maendeleo hayana chama.

Katika ziara hiyo ambayo mkuu huyo wa wilaya aliongozana na wataalama mbalimbali toka halmashauri walishirikiana na wananchi kufanya usafi katika barabara.

Mwisho………..

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ufahamu ugonjwa wa Ngiri ( Hernia) kiundani zaidi

Mama ajifungua mapacha wenye baba tofauti

UVCCM SIHA YAZINDUA KAMPENI YA KUGAWA TAULO ZA KIKE KATIKA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI