RC ATAKA MGAWANYO SAWA WA WALIMU KWA KILA WILAYA
MOSHI . MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO, DK. ANNE MGHWIRA (NA NNE KULIA WALIOKAA), KULIA KWAKE NI KATIBU WA CHAMA CHA WALIMU MKOA, DIGNA NYAKI PAMOJA NA MWENYEKITI WA CHAMA HICHO OMARY MCHOME WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WADAU MBALIMBALI WA ELIMU WAKATI WA KIKAO CHA KUPOKEA TAARIFA YA MRADI WA UBORESHAJI ELIMU KWA MPANGO WA MWALIMU MAHIRI (QUALITY EDUCATION THROUGH EXPERT TEACHER SYSTEM (QUEETS). MKUU wa mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anne Mghwira amewataka maafisa Elimu mkoa kwa shule za msingi na sekondari kuhakikisha wanafanya mgawanyo sawa wa walimu katika kila wilaya kwani wilaya za Mwanga na Same zinaupungufu mkubwa wa w...