RC ATAKA MGAWANYO SAWA WA WALIMU KWA KILA WILAYA
MOSHI.
MKUU wa mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anne Mghwira
amewataka maafisa Elimu mkoa kwa shule za msingi na sekondari kuhakikisha
wanafanya mgawanyo sawa wa walimu katika kila wilaya kwani wilaya za Mwanga na
Same zinaupungufu mkubwa wa walimu tofauti na wilaya nyingine za Kilimanajro.
Dk. Mghwira alitoa kauli hiyo jana,
katika kikao cha wadau mbalimbali wa Elimu kilichokuwa kikipokea taarifa ya
Mradi wa uboreshaji wa Elimu kwa mpango wa Mwalimu mahiri (Queets), ambapo
alisema kuwa zipo shule katika wilaya ya Mwanga na Same zinawalimu wawili paka
watatu huku katika wilaya ya Hai na Siha kukiwa na idadi kubwa ya walimu.
Alisema kuwa, idadi hiyo ndogo ya
walimu katika baadhi ya shule wilayani Mwanga na Same imekuwa ikichangia
wanafunzi kufanya vibaya hali ambayo imepelekea kwa sasa wazazi kuanza
kulalamikia tatizo hilo la uchache wa walimu.
“Maafisa Elimu mkoa mnapaswa kuangilia
tatizo hilo la uhaba wa walimu katika wilaya ya Mwanga na Same na kulitafutia
ufumbuzi haiwezekani wilaya ya Hai na Siha zina na walimu wengi alafu zipo
walaya ambazo hazina walimu ifike mahali sasa muone umuhimu wakuwahamisha
walimu wengine kwenda kwenye hizo wilaya zenye upungufu” alisema Dk. Mghwira.
Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa, Mradi
huo wa Queets ambao katika mkoa wa Kilimanjaro unatoa huduma katika Halmashauri
tatu za Moshi vijijini, Moshi manspaa na Hai, umekuwa na changamoto kubwa ya
kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Alitumia nafasi hiyo kuwaomba
wafadhili wa mradi huo kuona umuhimu wa kufikia katika halmashauri zote za mkoa
wa Kilimanjaro ili kuwasaidia walimu kujifunza mbinu na ujuzi wa kuwafundisha
wanafunzi ili kuufanya mkoa wa Kilimanjaro kuendelea kuwa kinara katika Elimu.
Aidha Dk. Mghwira aliwataka Walimu
kuisaidia jamii kurudi katika ualisia wa Uafrika na tamaduni zake na kuacha
tabia ya kuiga tamaduni zinazopotosha na kuharibu ualisia wa Muafrika.
Kwa
upande wake, Meneja wa mradi wa Queets, Donatian
Marusu alisema kuwa mradi huo unafadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la
Helvetas Swiss Inter-cooperation (HELVETAS), ambapo hujishughulisha na maswala
ya Elimu na Kilimo.
Marusu alisema kuwa, kutokana na tafiti mbalimbali za elimu hapa
nchini ikiwamo ya UNESCO ya mwaka 2010, ilibainika kuwa kuendelea kushuka kwa
kiwango cha elimu ya msingi kumechangiwa na kukosekana kwa mafunzo ya uhakika
kwa Walimu kazini.
Alisema kuwa shirika la Helvetas kwa kushirikiana na chama cha
Walimu Tanzania (CWT), waliamua kuanzisha mradi wa Queets
kwa kutoa mafunzo kwa walimu kwa masomo ya Hisabati, Lugha ya Kiingereza na
elimu ya Sayansi ya mazingira katika wilaya za Hai na Moshi kwa mkoa ya
Kilimanjaro, Arusha na Manyara.
“Hadi kufikia mwaka 2017 walimu bobezi wapatao 6,612 kutoka katika
shule 1800 za mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara wamefundishwa kwenye
mbinu na rahisi za ufundishaji pamoja na utengenezaji wa zana za kufundishia na
kujifunzia zinazotokana na mazingira wanayoishi” alisema Marusu.
Aidha Meneja mradi huo alibainisha kuwa, jumla ya Walimu wakuu wa
shule za msingi wapatao 1,438 na maafisa Elimu kata 266 wameoatiwa mafunzo ya
usimamizi na ufuatiliaji wa mradi huo wa Queets.
Alisema kuwa, wanafunzi wapatao 718,000 kutoka katika shule za
mradi wameweza kufaika na mardi huo kupitia walimu wao walionufaika na elimu
hiyo, huku pia shule hizo zimegawiwa jumla ya vitabu vya ziada 10,627 vya
masomo ya Hisabati, Kiingereza na Sayansi ya mazingira.
Marusu alisema changamoto wanazokabiliana nazo ni pamoja na baadhi
ya walimu kutofikisha maarifa na ujuzi waliopata kwa walimu wenzao, pia
kumekuwa na ufuatiliaji hafifu kutoka halmashauri ili kuhakikisha kuwa walimu
wanatekeleza majukumu waliyopewa wakati wa mafunzo.
Mwisho


Maoni
Chapisha Maoni