Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2018

WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA SIASA CHAFU

Picha
                                                                    MOSHI. MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI YA KIDATO CHA SITA KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA MAWENZI, MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAZAZI MKOA WA KILIMANJARO, DAUDI MRINDOKO (katikati), AKIWA NA MKUU WA SHULE YA SEKONDARI YA MAWENZI  CHRISTINE SHIRIMA (kushoto), NA KULIA NI MWENYEKITI WA BODI YA SHULE HIYO PROFESA CHAMBO. WAHITIMU wa kidato cha sita mwaka 2018, nchini wameshauriwa kuacha tabia ya kufanya siasa chafu pamoja na biashara haramu ya madawa ya kulevya na badala yake watumie elimu waliyoipata katika kushirikiana na Serikali kuleta maendeleo. Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro, Daudi Mrindoko katika mahafali ya 26 ya kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Mawenzi iliyopo manisp...

UVCCM KILIMANJARO:Maalim Seif Ujiuzulu siasa umechoka

KILIMANJARO. Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Mkoa Kilimanjaro  umesema siasa za maji taka, uongo fitna na majungu, zimepitwa na wakati hivyo umemtaka Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akubali kiungwana kujiuzulu siasa na kupumzika. Umeeleza kuwa Mwanasiasa huyo hadi leo kubaki kwenye ulingo wa siasa wakati wenzake wengi wameachia ngazi ,yaonyesha ana ajenda ya siri ambayo mtu mwingine ndani ya CUF hana siri hiyo . Matamshi hayo yametamkwa jana na Katibu  wa UVCCM Mkoa Kilimanjaro Abdulrahim Hamid  alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu tuhuma dhidi ya Makamo wa Rais Mama Samia zilizotolewa na Maalim Seif hivi karibu wakati akiwa mkoa Kusini Unguja . Hamid alisema kama yupo mwanasiasa mwenye vyama viwili Zanzibar hawezi kuwa mbele ya Maalim Seif kwani ndiye mwanasiasa mwenye vigezo vyote vya kuwa na imani ya kisiasa na kadi mbili kwa wakati mmoja . Alisema si jambo la kawaida kama kweli Maalim Seif si rafiki wa serikali za CCM aweze kuingia kwenye vikao maz...

Mwigizaji wa India Salman Khan ahukumiwa kufungwa jela kwa kosa la uwindaji haramu

Picha
Khan anauwezo wa kukata rufaa Mahakama moja ya India imemhukumu nyota muigizaji wa sinema za Bollywood Salman Khan, hukumu ya miaka mitano jela kwa kuua aina mojawepo ya swala ambao ni adimu kupatikana duniani mwaka 1988. Mahakama hiyo iliyoko Jodhpur imemtoza faini ya rupia 10,000 ($154; £109) kwa kosa hilo. Amepelekwa korokoroni na anatarajiwa kusalia huko kwa muda. Khan aliwaua swala wawili kwa jina blackbucks , ambao hulindwa na kuhifadhiwa, Magharibi mwa jimbo la Rajasthan alipokuwa akiigiza filamu. Zsa Zsa Gabor, mwigizaji aliyeolewa mara tisa Mwigizaji adai alitishiwa kuhusu madai ya kufanya ngono na Trump Waigizaji wengine wanne walioshiriki naye uigizaji kwenye filamu hiyo, waliokuwa wamehukumiwa kwa kosa hilo na mahakama ya awali, walisamehewa. Khan, 52 , anaweza kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo wa mahakama ya juu. Wanahabari wamesema atasalia korokoro...

Mbarawa awataka Wajumbe sekta ya Ujenzi kujitathimini

Picha
  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amewataka wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Sekta ya Ujenzi kujitathimini yale waliyoazimia kutekeleza kwa mwaka wa Fedha 2017/18 kama yamefikia lengo ili kuweza kusaidia kuboresha utendaji na kutafutia ufumbuzi masuala ambayo yanakwamisha ufanisi wa kazi na kuwezesha mazingira wezeshi kwa wafanyakazi. Prof. Mbarawa amesema hayo mkoani Morogoro, wakati akifungua kikao cha baraza la wafanyakazi ambapo pamoja na mambo mengime amesisitiza umuhimu wa baraza hilo katika kuhakikisha kuwa waajiri na watumishi wanatambua wajibu na haki zao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuleta matokeo chanya katika utendaji kazi wenye tija, staha na upendo. Ni matarajio yangu kuwa kila mjumbe kwa nafasi aliyonayo katika baraza hili atatumia fursa hii kutoa michango ya mawazo ili iweze kuwa mwongozo mzuri wa kutekeleza majukumu kwa ufanisi”, amesema Prof. Mbarawa. Aidha, ametoa wito kwa ...

Magufuli kuzindua ukuta ya mgodi ya madini ya Tanzanite leo

Picha
  Rais John Magufuli wa Tanzania, leo anatarajiwa kuzindua ukuta ya mgodi ya madini ya Tanzanite,iliopo eneo la Mererani, kaskazini mwa nchini Tanzania Ukuta huo wenye urefu wa kilomita 24.5 na urefu wa mita tatu kwenda juu, umejengwa kufuatia agizo lililotolewa na Rais John Magufuli, kama jitihada za kudhibiti na kuzuia utoroshwaji wa madini hayo, ambayo yanapatikana nchini Tanzania pekee. Awali, Mwezi Februari , wakuu wa vyombo vya usalama, walitembelea eneo hilo, kuukagua ukuta huo uliojengwa kwa gharama za Kitanzania isiyozidi bilioni 6. Walisisitiza kuwa lengo la kujengwa kwake ni kuzuia uhalifu na si kuwazuia wachimbaji wakubwa na wadogo kupata riziki zao. Wakitoa taarifa kwa viongozi wa ulinzi, wataalamu waliojenga ukuta huo, walisema licha ya kufanikisha ujenzi huo, changamoto mbalimbali walikutana nazo ikiwemo hatari inayo ukabili ukuta huo, kutokana na wachimbaji ku...

Cecilia Pareso aseama kama mnataka futeni yu Vyama vya Upinzani

Picha
  Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Cecilia Pareso amesema kama serikali ina lengo la kuwabana na kuwanyima haki wapinzani, basi ni bora mfumo wa vyama vingi ukafutwa ili ifahamike kwamba nchi ni ya chama kimoja. Pareso ameyasema hayo jana Aprili 5, Bungeni Mjini Dodoma wakati akichangia katika Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 2018/19 huku akidai kwamba vyama vya upinzani vimekuwa vikionewa ikiwemo viongozi wake kukamatwa mara kwa mara na kufunguliwa mashtaka huku wengine wakifungwa jela. Amesema vyama hivyo vimekuwa ni adui mwingine kwa kuwa kwa sasa vinapigwa vita na Serikali iliyopo madarakani, kuzuiwa kufanya shughuli za siasa majukwaani. Pia alidai chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni, zilikuwa ni kati ya Chadema na Jeshi la Polisi na kudai kwamba wabunge na madiwani walinunuliwa, wakahama vyama vyao, hivyo kukalazimika kufanyika chaguzi nyingine ndogo alizodai zimegharimu zaidi ya Sh bilioni 6. “Kama mnakataza vyama v...